Na Livingstone Mkoi
Katika hali isiiyokuwa ya kawaida mwanamuziki Lucas Mkenda maarufu kwa jina la Mr Nice ameibuka na kueleza sababu zilizomfanya kufirisika licha ya kuwahi kumiliki zaidi ya bilioni moja na nusu kwenye akaunti zake tofauti.
Akiongea na Xdeejayz Tanzania mwanamuziki huyo ambae kwa sasa yupo nchini kwa muda mfupi kabla ya kurudi tena nchini Kenya alikohamishia makazi na kufanyia shughuri zake za kimuziki huko.
Akizungumza na mwandishi wetu kwenye ukumbi wa mpya wa burudani wa Full Stop uliopo Mwanamboka Kwa Manyanya Kinondoni Jijini Dar ambapo alisema kuwa dunia imemfanyia kitu kibaya na hafahamu nini kimetoka katika maisha yake.

Mr Nice alisema kuwa anashindwa kuelewa kwa nini maisha yamempiga kiasi hicho kwani pesa yote aliyokuwa anaipata alikuwa anaipata kwa jasho lake” Kaka naweza kusema hii ni mipango ya Mungu tu kwani sikuwahi kumdhurumu mtu wala kuiba cha mtu pesa yote nilikuwa naipata kwa hali naweza kusema hii ni mipango ya Mungu tu wala si mkono wa mtu” Alisema mwanamuziki huyo

Aidha mwanamuziki huyo anasema” Niliwahi kumiliki zaidi ya milioni elfu moja na mia tano kwenye bank tofauti hapa nchini pesa hizo zilitokana kufanya shoo nyingi za nje ya nchi kama Marekani, Uingereza, Ujerumani, Sweden, Holand, Dubai, Afrika Kusini na kwingineko na kila shoo nilikuwa napata pesa ndefu sana” Alisema
Hata hivyo Mr Nice nasema kuwa hizo ni nchi za mbali  lakini bado shoo za alizokuwa anazifanya nchi za Kongo, Zambia, Uganda, Rwanda, Kenya na moja ya shoo ambayo akiikumbuka huwa inamtoa machozi ni ile ya nchini Rwanda ambayo siku anashuka Airport alikuta kitu cha kushangaza sana.
Anasema alikuta umati mkubwa wa watu ukimsubiri pamoja na Waziri wa Michezo wa nchi hiyo pamoja maofisa wa ngazi za juu wa Polisi na Jeshi huku kukiwa na Red Capet kisha akapigiwa saluti huku akisindikizwa na mizinga ishirini na moja.Hata hivyo mwanamuziki huyo anasema alifikia uamuzi wa kujiita the milonea Mr Nice baada ya kuingia mkataba na kampuni ya TBL kupitia bia yake ya Safari alifanya shoo mikoa yote ishirini n tano kwa pesa ndefu na kufanya kuwa mwanamuziki mwenye pesa nyingi Afrika Masharki kuliko mwanamuziki yeyote.
Mambo mengine ya kushangaza aliyokuwa nayo mwanamuziki huyo kipindi akiwa na pesa ni juu ya msafara wake uliokuwa umejaa wapambe wengi na kulazimika kutumia magari zaid ya nane kwenye mizunguko yake huku yakiwa hayazimwi Ac masaa ishirini na nne hata kama hayana watu ndani.
Aidha Mr Nice alimaliza kusema kuwa anawashauri wanamuziki wa sasa kujifunza kwa waliopita ili nao yasijekuwakuta kama yaliyowakuta wao.
CREDIT:Swahilitz.info

0 comments:

Post a Comment

 
Top
Blogger Template